Tanzania emblem
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania

Ununuzi na Ugavi

Majukumu ya Kitengo cha Ugavi na Ununuzi

Mkuu wa Kitengo - Nessy E. Kyejo

  1. Kusimamia ununuzi wowote na uuzaji wa mali za Wizara kwa njia ya Zabuni isipokuwa usuluhishi na kutunuku zabuni ;
  2. Kuratibu shughuli za Bodi ya Zabuni ya Wizara;
  3. Kutekeleza maamuzi ya Bodi ya Zabuni ya Wizara;
  4. Kufanya kazi kama Sekritarieti ya Bodi ya Zabuni ya Wizara
  5. Kuandaa mpango wa Ununuzi na Uuzaji wa mali za Wizara kwa njia ya Zabuni;
  6. Kupendekeza ununuzi na uondoshaji wa mali za Wizara kwa utaratibu wa zabuni;
  7. Kukagua na kuainisha upungufu wa mahitaji katika Wizara na kutoa tamko kuhusu mahitaji hayo;
  8. Kuandaa nyaraka za zabuni kwa ajili wazabuni kushiriki;
  9. Kuandaa matangozo ya fursa za zabuni;
  10. Kuandaa rasmu za Mikataba;
  11. Kutoa mikataba iliyothibitishwa na kusainiwa;
  12. Kuandaa na kuhifadhi kumbukumbu za mchakato wa ununuzi na uuzaji wa mali za Wizara;
  13. Kuandaa na kutunza orodha au kitabu cha mikataba yote ambayo Wizara imetunuku;
  14. Kuandaa taarifa za kila mwezi kwa ajili ya Bodi ya Zabuni ya Wizara;
  15. Kuandaa taarifa ya kila robo ya mwaka juu ya utekelezaji wa mpango wa ununuzi na kuwasilisha katika kikao cha menejimenti ya Wizara;
  16. Kuratibu kazi za ununuzi na uondoshaji wa mali za serikali katika Idara na vitengo vyote vya Wizara; na
  17. Kuandaa taarifa nyinginezo kadri zitakavyo hitajika muda wowote.