Tanzania emblem
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania

Ununuzi na Ugavi

Majukumu ya Kitengo cha Ugavi na Ununuzi

  1. Kusimamia ununuzi wowote na uuzaji wa mali za Wizara kwa njia ya Zabuni isipokuwa usuluhishi na kutunuku zabuni ;
  2. Kuratibu shughuli za Bodi ya Zabuni ya Wizara;
  3. Kutekeleza maamuzi ya Bodi ya Zabuni ya Wizara;
  4. Kufanya kazi kama Sekritarieti ya Bodi ya Zabuni ya Wizara
  5. Kuandaa mpango wa Ununuzi na Uuzaji wa mali za Wizara kwa njia ya Zabuni;
  6. Kupendekeza ununuzi na uondoshaji wa mali za Wizara kwa utaratibu wa zabuni;
  7. Kukagua na kuainisha upungufu wa mahitaji katika Wizara na kutoa tamko kuhusu mahitaji hayo;
  8. Kuandaa nyaraka za zabuni kwa ajili wazabuni kushiriki;
  9. Kuandaa matangozo ya fursa za zabuni;
  10. Kuandaa rasmu za Mikataba;
  11. Kutoa mikataba iliyothibitishwa na kusainiwa;
  12. Kuandaa na kuhifadhi kumbukumbu za mchakato wa ununuzi na uuzaji wa mali za Wizara;
  13. Kuandaa na kutunza orodha au kitabu cha mikataba yote ambayo Wizara imetunuku;
  14. Kuandaa taarifa za kila mwezi kwa ajili ya Bodi ya Zabuni ya Wizara;
  15. Kuandaa taarifa ya kila robo ya mwaka juu ya utekelezaji wa mpango wa ununuzi na kuwasilisha katika kikao cha menejimenti ya Wizara;
  16. Kuratibu kazi za ununuzi na uondoshaji wa mali za serikali katika Idara na vitengo vyote vya Wizara; na
  17. Kuandaa taarifa nyinginezo kadri zitakavyo hitajika muda wowote.