Tanzania emblem
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania

Fedha na Uhasibu

Mkuu wa Kitengo - Margareth Ndebelamatwi

Majukumu ya Kitengo cha Fedha na Uhasibu

  1. Kutekeleza jukumu la ulipaji fedha kwa kuzingatia taratibu na miongozo iliyopo na kuhakikisha watu wanafuata sheria na taratibu za fedha kwa makundi mbalimbali yakiwemo;
    • Madai ya watumishi na stahili zao mfano malipo ya likizo, safari na madai mengineyo.
    • Kulipa stahili za viongozi kisheria
    • Kulipa mishahara
    • Madai mbalimbali ya viongozi mfano fedha ya safari
    • Kulipa watoa huduma mbalimbali zilizotokana na mikataba mfano, ulinzi, usafi, huduma za internet, simu, umeme na kadhalika
    • Kulipa gharama ya matengenezo ya magari na vifaa mbalimbali vya ofisi
    • Kulipia ,manunuzi mbalimbali mfano shajala na kadhalika
  2. Utunzaji wa kumbukumbu na nyaraka za fedha
  3. Kuandaa taarifa za kila mwezi, kila robo ya mwaka, nusu mwaka na kuwasilisha Hazina
  4. Kuandaa taarifa za hesabu kwa mwaka mzima wa fedha “Annual Final Accounts”
  5. Kutoa majibu na kufuatilia majibu toka Idara mbalimbali na Vitengo kutokana na Hoja za Ukaguzi, hii inahusu hoja za mkaguzi wa ndani na nje
  6. Kuandaa majibu kutokana na “Management letter” anayoitoa Mkaguzi wa Nje, kutokana na utendaji wa mwaka mzima wa wa Wizara kwa Idara na Vitengo vyote.
  7. Ufuatiliaji wa masuala ya PAC endapo Wizara itatakiwa kuhudhuria mbele ya Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali.
  8. Utoaji taarifa kuhusu maduhuli yaliyokusanywa na Wizara
  9. Kusimamia vikao viwili kabla na baada ya Ukaguzi (Entry and Exit Conference)
  10. Usimamizi wa Special Funds kama zipo
  11. Kutoa ushauri kwa Afisa Masuhuli kuhusiana na Masuala ya fedha.