Tanzania emblem
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania

Utafiti wa Sheria

Mkuu wa Kitengo - Juliana E. Munisi

Majukumu:

  1. Kufanya utafiti wa awali na kupendekeza maeneo yanayohitaji maboresho ya kisheria.
  2. Kuandaa andiko la awali, Taarifa ya majadiliano na taarifa yenye mapendekezo ya maboresho ya sheria.
  3. Kufanya utafiti kwa ajili ya maboresho ya sheria.
  4. Kuainisha na kuchambua taarifa za kisheria zilizoandaliwa na taasisi nyingine, wataalamu elekezi na taarifa za watafiti wa kisheria zenye mlengo wa maboresho ya kisheria.
  5. Kushauri Taasisi za Serikali katika masuala yanayohitaji maoni ya /msaada wa kisheria.
  6. Kutathmini mikataba mbalimbali iliyoridhiwa na Serikali, makubaliano, itifaki na nyaraka nyinginezo za kikanda na kupendekeza kwa Serikali namna ya kuziasili.
  7. Kuratibu program za mabadiliko ya kisheria yanayoendelea ambayo yanaendana na programu za shughuli za Tume.
  8. Kuendesha warsha na makongamani yanayohusiana na maboresho ya sheria.