Katibu Mtendaji wa Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania Bw. George Mandepo akipokea Tuzo aliyokabidhiwa na Bi. Jackline Nungu kwa niaba ya Watumishi wa Tume hiyo ikiwa ni kutambua mchango wake mkubwa katika kuimarisha utendaji kazi, ushirikiano na maendeleo ya watumishi ndani ya Tume hiyo. Tuzo hiyo ilitolewa Mei 14,2026 na watumishi wakati wa Kikao cha Baraza la 24 la Wafanyakazi lililofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Tume ya Utumishi wa Mahakama uliopo mjini Dodoma .